kuadhimisha Siku ya Hedhi Duniani
Katika kuadhimisha Siku ya Hedhi Duniani, Mwanamke Initiatives Foundation (MIF) iligawa Taulo za Kike 500 kwa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Bi. Siti Abasi Ali na 500 nyengine alikabidhiwa Afisa Elimu Wilaya ya Magharibi B, kwa wanafunzi wa kike katika shule za wilaya ya Magharibi.
Jumla ya Taulo zote ni 1000.
Hii ni sehemu ya dhamira yetu ya kuhakikisha mtoto wa kike anapata mazingira salama, heshima na utulivu wa kujifunza ili aweze kufikia ndoto zake bila kukatishwa tamaa na changamoto za hedhi.